Uthibitishaji Ubora wa Bidhaa
TARATIBU ZA KUPATA ALAMA YA UBORA
Zipo hatua mbalimbali ambazo mzalishaji hupaswa kuzingatia kabla ya kupata leseni ya kutumia alama ya ubora ya TBS kwenye bishaa yake.
1. Maombi
Maombi ya kupata alama ya ubora wa bidhaa hufanywa na muombaji kupitia mfumo wa kielektroniki (i-SQMT) unapatikana kupitia tovuti ya TBS (www.tbs.go.tz) kwenye kitufe cha e-service au moja kwa moja kupitia linki ya https:// portal.tbs.go.tz Baada ya maombi kukamilika tarehe ya ukaguzi wa awali hupangwa. izingatiwe kuwa mwenye kiwanda anatakiwa kuwa katika uzalishaji siku ya kufanya ukaguzi wa awali.
2. Ukaguzi wa Awali
Ukaguzi wa awali hufanywa na wakaguzi wa TBS. Sampuli huchukuliwa na kupimwa ili kuona kama bidhaa inakidhi matakwa ya kiwango husika. Mkaguzi huandaa taarifa kuhusu hali halisi ya kiwanda na mambo yanayostahili kurekebishwa.
3. Upimaji
Upimaji Sampuli zilizochukuliwa hupimwa katika maabara za TBS kwa kufuata kiwango husika. Baada ya kazi ya upimaji kumalizika, ripoti hutolewa kwa mwombaji.
4. Utoaji wa Leseni
Utoaji wa Leseni Uamuzi kuhusu kutoa au kutotoa leseni ya kutumia alama ya ubora hutegemea tu ripoti ya ukaguzi wa awali wa kiwanda pamoja na ripoti ya maabara. Kimsingi ripoti zote mbili zinatakiwa kuonyesha kwamba mazingira ya uzalishaji kiwandani, mfumo wa uzalishaji na bidhaa iliyopimwa havina matatizo. Ikiwa sivyo basi mzalishaji hutakiwa kufanya marekebisho na baadaye mkaguzi wa TBS hutumwa tena na kuleta sampuli nyingine.
5.Uhakiki wa Leseni/Cheti
Leseni ya alama ya viwango/cheti cha bidhaa iliyopimwa vitakuwa halali kwa mwaka mmoja tu. Mwisho wa kila mwaka mteja atatakiwa kuomba kuongezewa muda. Hatua hii itahakikisha kuwa kila mteja aliyethibitishwa ana zingatia sheria. Katika sehemu hii mteja atakaguliwa mara moja kwa mwaka iwapo kwa bahati mteja huyo amekosa kukaguliwa baina ya kipindi hicho.
Masharti ya Huduma ya Bure ya Uthibitisho wa Bidhaa kwa Wajasiriamali wanaoanza,wadogo wadogo na wa kati (MSMES)
Kila mwaka Serikali hutenga fedha kuwasaidia wajasiriamali wanaoanza, wadogo wadogo na wa kati (MSMES) wakati wanapoomba uthibitisho wa bidhaa zao ili wapate leseni ya kutumia alama za viwango vya ubora vya TBS. Baadhi ya wajasiriamali hao hawastahili kulipa ada yoyote kutokana na mtaji wao mdogo. Hata hivyo ili bidhaa zao ziweze kuthibitishwa chini ya mpango wa ruzuku ya serikali, SMEs wanatakiwa wapate barua ya utambulisho kutoka ofisi ya karibu ya Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO). Ni muhimu kuhakikisha kuwa barua hiyo inafafanua kile anachofanya mjasiriamali anayeomba.
Kwa maelezo zaidi kuhusu
utaratibu wa mpango wa leseni ya alama za viwango na cheti cha bidhaa
iliyopimwa, pakua jalada lifuatalo:
utaratibu wa kupata leseni ya alama ya ubora na cheti cha ubora wa bidhaa